HII NDO SABABU YA SIMBA SPORT CLUB KUKATA RUFAA MECHI YA KAGERA SUGER


 
 
 Unaweza kusema mambo yamekucha baada ya uongozi wa klabu ya Simba, kuwasilisha rufaa Bodi ya Ligi Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ukidai pointi za mchezo dhidi ya Kagera Sugar uliochezwa kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, Jumamosi.

Katika mechi hiyo, Simba ilipoteza kwa kufungwa mabao 2-1, lakini Simba inadai Kagera Sugar walimchezesha beki  Mohammed Fakhi akiwa ana kadi tatu za njano.
Kamati ya masaa 72 inatarajiwa kukutana kesho na imeelezwa tayari Simba ilishawasilisha rufaa hiyo.
Hata hivyo, Kagera Sugar imesisitiza kuwa Fakhi alikuwa na kadi mbili za njano.
Awali, Kocha Mecky Maxime alisisitiza gilo lakini Mohammed Hussien naye akasisitiza wana uhakika Fakhi ana kadi mbili za njano.
Katika mechi hiyo, Fakhi aliyewahi kuichezea Simba, alikuwa mmoja wa mabeki vizingiti dhidi ya washambuliaji wa Simba.
Ilikuwa ni mechi ya ushindani na Kagera walionyesha soka safi na kuishinda Simba.

Share :

Facebook Twitter Google+
0 Komentar untuk "HII NDO SABABU YA SIMBA SPORT CLUB KUKATA RUFAA MECHI YA KAGERA SUGER"

Back To Top