NAFASI ZA KAZI/ AJIRA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA



Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba anapenda kuwatangazia wananchi wote nafasi za kazi kwa kada mbalimbali kama ifuatavyo hapa chini
DEREVA: NAFASI 1
MAJUKUMU
i. Kuendesha magari ya abiria na malori
ii. Kuhakikisha gari na vyombo vyake vipoo katika hali  nzuri  wakati wote  na kufanya uchunguzi wa gari kabla na baada ya safari ili kugundua ubovu unaohitaji matengenezo
iii. Kufanya matengenezo madogo madogo katika gari
iv. Kutunza na kuandika daftrai la safari LOG – BOOK kwa safari zote
SIFA ZA MWOMBAJI
i. Awe na elimu ya kidato cha 4 au 6
ii. Mwenye lesseni ya daraja “C” pamoja na uzoefu wa kuendesha magari kwa muda usiopungua miaka mi 3 bila kupata ajali
iii. Mwenye cheti cha majaribio ya ufundi daraja la II
iv. Mwombaji asiwe na umri unaozid miaka 45
N
GAZI YA MSHAHARA TGOS A
DEREVA MASHUA/KIVUKO DARAJA LA II -  NAFAI I
MAJUKUMU
- Kufunga na kufungua kamba za mashua
- Kuchunga usalama wa abiria na magari yaliyomo ndani ya kivuko
- Kupanga abiria na magari ndani ya kivuko
- Kuendesha na kuongoza kivuko
- Kutunza daftari la safari za kivuko
- Kuhakiki kuwa inijini za kivuko zipo katika hali nzuri  ya kufanya kazi
- Kuangalia mafuta na vyombo vingine vya kufanyia kazi
SIFA ZA MWOMBAJI
- Awe na elimu ya kidato cha 4 au 6
- Awe na ujuzi wa kuendesha na kutunza kivuko uliothibitishwa na chuo cha DSM MARINE  INSTITUTE  na chuo kingine  kinachotambuliwa na serikali  kwa muda usiopungua miaka miwili
- Awe amefuzu mafunzo ya miezi 6 ya uokoaji wa maisha majini , kuogelea na kupanga watu na magari kwenye kivuko
NGAZI YA MSHAHARA TGOS A
KATIBU MAHSUSI DARAJA LA III NAFASI  1
MAJUKUMU
a. Kuchapa barua , nyaraka na taarifa za kawaida
b. Kusaidia kupokea wageni, kuwasaili shida zo na kuwaelekeza sehemu wanapoweza kushughulikiwa
c. Kusaidia kutunza  taarifa/kumbukumbu za matukio, miadi, tarehe za vikao,  safari za mkuu wake na ratiba yake ya kazi zingine zilizopangwa kutekelezwa katika ofisi anayofanyia kazi  na kumuarifu  mkuu wake kwa wakati unaohitajika
d. Kusaidia kutafuta na kumpatia mkuu wake majalada , nyaraka au chochote kinachohitajika katika shughuli za kazi hapo ofisini
e. Kusaidia kufikisha maelezo ya mkuu wake  wakazi kwa wasaidizi wake na pia  kumuarifu kuhusu taarifa  zozote anazokuwa amepewa na wasaidizi wao
f. Kusaidia kuyapokea majalada na kuyagawa kwa maofisa  walio katika sehemu  alipo na kuyakusanya , kuyatunza na kuyarudisha sehemu husika
g. Kutekeleza kazi zozote atakazokuwa amepangiwa na msaidizi wake wa kazi
SIFA ZA MWOWOMBAJI
a.

Awe na elimu ya kidato cha 4 au 6

b. Awe amehitimu mafunzo ya  uhazili na kufahulu hatua ya 3 ya somo la hatimkato la Kiswahili na kingereza  maneno 80 kwa dakika  moja
c. Awe amepta mafunzo ya kompyuta  kutoka chuo chochote kinachotambuliwa na serikali  na kupata cheti  katika program  za windows  Ms Office, internet, E-mail na Publisher
d. Mwombaji asiwe na umri  uliozod miaka 45
NGAZI YA MSHAHARA TGS B
MSAIDIZI WA KUMBU KUMBU DARAJA LA II NAFASI 1
MAJUKUMU
• Kutafuta kumbukumbu/nyaraka /mafaili yanayohitajika na wasomaji
• Kuthibiti upokeaji na uandikishaji wa kumbukumbu/nyaraka
• Kuchambua , kuorodhesha na kupanga kumbukumbu /nyaraka  katika makundi kulinganna na somo husika  kwaajili ya matumizi ya ofisi 
• Kuweka na kupanga kumbukumbu / nyaraka katika reki/file  racks cabinet  katika masijala
• Kuweka barua/kumbukumbu katika mafaili
• Kuchambua na kutafsiri  kumbukumbu  kwaajili ya mipango na huduma za ofisi
• Kutunza/kudhibiti na kutoa kumbukumbu za halmashauri
SIFA ZA MWOMBAJI
• Awe na elimu ya kidato cha 4 au cha 6
• Awe amefuzu  mafunzo ya cheti cha utunzaji kumbukumbu katika moja wapo ya fani za afya, masijala, mahakama na ardhi
• Mwombaji awe na umri usiopungua miaka 45
NGAZI YA MSHAHARA TGS B
MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III NAFASI - 4
MAJUKUMU 
i. Afisa msuluhishi na mtendaji  mkuu wa Serikali  ya kijiji
ii. Kusimamia ulinzi na usalma wa raia na mali zao kuwa mlinzi wa Amani  na msimamizi wa utawala bora katika kijiji
iii. Kuratibu na usimamia  upangaji wa maendelo ya kijiji  kuratibu mikutano ya kamati zote za Halmashauri ya kijiji
iv. Kutafsiri na kusimamia sera, sharia na taratibu
v. Kusimamia, kukusanya, na kuhifadhi kumbukumbu zote na nyaraka za kijiji
vi. Mwenye wa kikao ch wataalamu walipo katika kijiji
vii. Kupokea, kusikiliza, na kutatua  malalamiko na migogoro ya wananchi
viii. Kusimamia utungaji wa sharia  ndogo za kijiji
ix. Atawajibika kwa mtendaji wa kata
SIFA ZA MWOMBAJI
i. Awe na elimu ya kidato cha 4 au 6
ii. Awe amehitmuu mafunzo ya stashahada ya cheti katika moja ya fani zifuatazo utawala, elimu ya jamii, sharia, usimamizi wa fedha, maendeleo ya jamii, na sayansi ya Sanaa kutoka chuo kikuu Hombolo au chuo chochote kinachotambulika na serikali
iii. Mwombaji asiwe na umri chini ya miaka 45
NGAZI YA MSHAHARA TGS B
UTARATIBU WA KUTUMA MAOMBI
 Barua za maombi ziandikwe kwa mkono
 Barua ziandikwe kwa 
MKURUGENZI MTENDAJI WILAYA,
HALMASHAURI YA WILAYA,
S.L.P 131
MULEBA
 Muombaji aambatanishe
- CV, yenye namba za simu za kuaminika na wwadhamini watatu wa kuaminika
- Nakala za vyeti vya elimu ya sekondari na chuo
- Hati ya kuzaliwa
- Leseni ya udereva  kwa watakao omba udereva
- Picha moja ya passport size
MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA
- Waombaji wawe raia wa Tanzania
- Barua za uthibitisho wa matokeo  ya mithani  result slip na tesmonials  procisional  hazitapokelewa
- Wale ambao ni watumishi  wa barua zao  maombi zipitie kwa waajiri wao
- Waombaji waliosoma nje  ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa TCU NA NECTA
- Waombaji waliotaifishwa  katika utumishi wa umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wanakibali cha utumishi wa katibu mkuu kiongozi
- Uwasilishaji wa taarifa za kughushi ni  wahusika watachukuliwa hatua za kisheria
- Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 09/09/2017


Share :

Facebook Twitter Google+
0 Komentar untuk "NAFASI ZA KAZI/ AJIRA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA"

Back To Top